• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 12:38 PM
Mpenzi wangu ataka nitafute mwanamume mwingine maana amefutwa kazi!

Mpenzi wangu ataka nitafute mwanamume mwingine maana amefutwa kazi!

SHANGAZI;

Mpenzi wangu amekuwa akinisaidia kulea mtoto tuliyezaa pamoja. Aliachishwa kazi mapema mwaka huu anataka tuachane kwa sababu hana uwezo wa kunisadia. Ananiambia nitafute mwanamume mwingine. Nimechanganyikiwa, nishauri.

Ni jambo la kushangaza kwamba mwanamume uliyemzalia akidai kukupenda sasa anakwambia utafute mwingine ili akusaidie kulea mtoto wenu. Hiyo ina maana kwamba utabeba mzigo huo peke yako kwani na huwezi kumlazimisha.

Tumeishi miaka 2 lakini moyo umemkataa

Niliingia katika uhusiano wa kimapenzi na mwanamume ambaye sikuwa na hisia kwake nikidhani hatimaye ningempenda. Huu ni mwaka wa pili na moyo umemkataa. Nifanyeje?

Huo ni ulaghai wa kimapenzi. Ulimhadaa mwanamume huyo kuwa unampenda na atavunjika moyo sana akijua huna hisia kwake. Usiendelee kumpotezea wakati. Mwambie ukweli ili muachane atafute mwingine.

Mwanaume anipotezea wakati bure, simpendi

Huu ndio mwaka wangu wa pili katika uhusiano wa kimapenzi. Nimefikiria sana kuhusu mwanamume niliye naye kugundua nimepoteza wakati wangu bure kwani sijaona lolote la maana kwake. Nishauri.

Msimamo wako ni kuwa humpendi mwanamume huyo na hutaki kuendelea na uhusiano huo. Usipoteze wakati zaidi, ukweli huo ili muachane kila mmoja wenu aendelee na maisha yake.

Kila nikipomwitaji huwa ananihepa licha ya kujitolea kwangu kwake

Nina mpenzi na ninampenda kwa dhati. Nimekuwa nikijitolea kwa ajili yake kila anaponihitaji. Lakini nikimhitaji kimahaba hunihepa kupitia vijisababu. Nahisi kuwa hanipendi. Nishauri.

Wapenzi wa dhati wanafaa kusaidiana kwa kila hali. Kama mpenzi wako akikuhitaji huwa unapatikana ili kumfaa, inafaa kuwa hivyo kwake. Tabia yake hiyo ni dalili kuwa hakupendi. Kama unahisi hakupendi achana naye.

  • Tags

You can share this post!

Apu na teknolojia za kidijitali kuboresha kilimo na ufugaji

Maandalizi ya Maonyesho ya ASK Nairobi 2023 yakamilika

T L