• Nairobi
  • Last Updated May 12th, 2024 10:50 AM
Mwanahabari wa KBC aporwa

Mwanahabari wa KBC aporwa

Na SYLVANIA AMBANI

MWANAHABARI mmoja wa Shirika la Utangazaji nchini (KBC) alishambuliwa na kuibiwa na vijana wasiojulikana akiwa kwenye trafiki ya barabara ya Globe.

Akizungumza na Taifa Leo kwa simu, Bi Shiksha Arora alieleza kuwa tukio hilo lilifanyika saa kumi na moja jioni akiwa anelekea katika sherehe ya uzinduzi wa stesheni ya KBC katika hoteli ya Serena, Jumatatu jioni.

Kijana mmoja alikigonga kioo cha gari lake na kukiacha kimeinama. Wakati alipokishusha kioo cha dirisha ili kukitengeza kioo hicho, kijana mwingine aliufungua mlango wa gari lake na kuingia ndani.“Jana karibu saa kumi na moja alasiri niliibiwa katika njia-panda ya Globe.

Kijana mmoja alikigonga kioo cha upande cha gari langu, naye mwingine akapata nafasi na kuufungua mlango wa gari na kujitoma ndani,” Bi Arora alieleza. Kijana aliyeingia katika gari lake alianza kumtishia akitaka apewe simu na begi.“Niliingiwa na uoga.

Kijana huyo alipoona kuwa sifanyi alivyotishia, alianza kuninyonga. Huo ndipo nilipoanza kupiga honi na kuvutia umakinifu wa wapita-njia, hali iliyofanya mwizi huyo kutoroka,” Bi Arora akaongeza.

Alishuku huenda wezi hao wanashirikiana kuwaibia watu mchana.Aliwaonya watu kutoteremsha vioo vya madirisha ya magari yao wakiwa katika trafiki. Kamanda wa polisi Kaunti ya Nairobi, Bw Augustine Nthumbi, aliwataka watu waripoti matukio kama hayo.

  • Tags

You can share this post!

Washukiwa 15 wa mauaji kuendelea kusota rumande

Rais kuzindua Safari Rally ulinzi mkali ukiwekwa