• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 5:44 PM
Mwanamume adai yeye ni yatima anayehitaji kuwa na watoto wengi asihatarishe kizazi

Mwanamume adai yeye ni yatima anayehitaji kuwa na watoto wengi asihatarishe kizazi

NA TITUS OMINDE

MWANAMUME mmoja ambaye alikiri shtaka la kumjeruhi mke wake pamoja na shemeji yake aliambia mahakama kuwa alimjeruhi mkewe kutokana na hasira baada ya kudai mke alilenga kuharibu ujauzito.

Mwanamume huyo aliambia hakimu mwandamizi wa Eldoret Nancy Barasa kwamba alipandwa na hasiria akidai mkewe alikuwa amepanga njama na dadake kufanikisha uavyaji wa mimba.

Edwin Barasa aliambia mahakama kuwa yeye ni yatima na anahitaji kuwa na watoto wengi ili familia yake ipanuke na awe na jamaa wa karibu.

“Ndiyo nakiri mashtaka yangu lakini hili lilitokana na ukweli kwamba mimi ni yatima na nahitaji watoto wengi,” aliambia mahakama huku akitokwa na machozi.

Mahakama iliambiwa kuwa mnamo Septemba 15, 2023, katika eneo la Kisumu Ndogo mtaani Langas mjini Eldoret, alimjeruhi mlalamishi na kumsababishia majeraha ya kudumu.

Akikiri mashtaka huku akisema alikuwa na machungu mengi ya hatari ya kutopata mtoto.

Bw Barasa aliambia mahakama kuwa alikuwa tayari kuonyesha polisi pahala ambapo inadaiwa mlalamishi kwenye kesi alizika kijusi.

Mahakama iliamuru maafisa wa kurekebisha tabia kumfanyia mahojiano kabla ya kuleta ripoti ya kifungo cha nje.

Kesi hiyo itatajwa mnamo Oktoba 3, 2023.

  • Tags

You can share this post!

Waislamu wakerwa na hatua ya mahakama kuwapa mashoga uhuru...

Man-U imeisha hakuna timu hapo, Ole Gunnar atoboka!

T L