• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 3:16 PM
Nimripoti mama kwa babangu? Sababu nilimuona akichepuka na jirani yetu

Nimripoti mama kwa babangu? Sababu nilimuona akichepuka na jirani yetu

SHANGAZI AKUJIBU:

Vipi shangazi? Nina miaka 19. Nimegundua mama yangu ana uhusiano wa kimapenzi na mwanamume jirani yetu. Baba anafanya kazi mbali na nyumbani. Nafikiria kumwambia. Nishauri.

Mama yako amefanya makosa kwa kuanzisha uhusiano wa kimapenzi nje ya ndoa yake. Lakini haitakuwa vyema kwako kuingilia maisha yake ya kibinafsi. Baba yako akijua wanaweza kuachana. Shughulika na maisha yako.

Jirani ameponyoka na mke wangu!

Hujambo shangazi? Juzi nilitoka kazini ghafla nikamfumania mwanamume jirani yetu nyumbani kwangu akiwa na mke wangu. Ni tajiri na ninaamini alimshawishi kwa pesa. Nafikiria kumchukulia hatua kisheria.

Sidhani hatua yako hiyo itafaulu. Jirani yako hakuingia nyumbani kwako kwa lazima. Pili, hakumlazimisha mke wako. Kama alitumia pesa au la, hiyo kamwe si hoja, bora tu walikubaliana.

 

Nataka kuwa ‘fisi’ jike

Shangazi pokea salamu zangu. Nilimuacha mpenzi miezi kadhaa iliyopita nilipogundua alikuwa na wanawake wengine. Nimeamua kulipiza kisasi kwa kuwacheza wanaume. Waonaje?

Sikubaliani na mpango wako huo. Ingawa mpenzi wako alikuvunja moyo, si vyema kulipiza kisasi dhidi ya wanaume wengine. Pili, ni hatari kuwa na wapenzi wengi kwani unaweza kuambukizwa magonjwa.

Bosi hanitakii mazuri

Hujambo shangazi? Mimi na mke wangu tunafanya kazi katika kampuni moja. Nimegundua kuwa bosi wetu anamtaka mke wangu kimapenzi. Nafikiria kumkabili lakini pia naogopa kufutwa kazi. Nishauri.

Kitendo cha bosi wenu ni ukiukaji wa maadili ya kikazi. Hasa, hiyo ni dhuluma ya kimapenzi kwa sababu anajua huyo ni mke wako. Usimuogope. Hawezi kukufuta kazi kwa kuwa anajua unaweza kumchukulia hatua kisheria.

  • Tags

You can share this post!

Afueni serikali ikiongezea wanafunzi muda kutuma maombi ya...

Lojing’i ya Nakuru ambayo haina walevi wala makahaba

T L