• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 7:50 AM
Polisi aua mpenzi wake na kujiua

Polisi aua mpenzi wake na kujiua

JOHN NJOROGE Na JOSEPH OPENDA

AFISA wa polisi alishangaza wakazi wa lokesheni ya Sarambei, Kuresoi North, kaunti ya Nakuru alipomuua mpenzi wake kwa kumpiga risasi kabla ya kujipiga risasi.

Bw Joseph Laurien Akorot, ambaye alikuwa naibu mkuu wa kituo cha polisi cha Mau Summit alisemekana kumuua mpenzi wake Bi Janet Chebet, 30, kabla ya kujipiga risasi. Alikufa akiendelea kupokea matibabu.

Kisa hicho kilitokea mwendo wa saa moja Jumatatu asubuhi.

Taarifa ya polisi ilisema kwamba afisa huyo alikuwa amemsindikiza mpenzi wake kutoka nyumba yake na baada ya kumfikisha aliondoka kisha akageuka na kumpiga risasi mgongoni.

  • Tags

You can share this post!

BENSON MATHEKA: Itatufaa sana tukiiga mawakili katika kesi...

Ngome za Raila zadumisha amani, utulivu

T L