• Nairobi
  • Last Updated May 6th, 2024 1:13 PM
Ngome za Raila zadumisha amani, utulivu

Ngome za Raila zadumisha amani, utulivu

NA WAANDISHI WETU

KULIKUWA na utulivu katika ngome ya kiongozi wa Azimio Raila Odinga ya Nyanza baada ya Mahakama ya Upeo kutupilia mbali kesi yake na kuidhinisha ushindi wa Rais mteule William Ruto.

Kinyume na ilivyobashiriwa, hakukuwa na fujo jiji la Kisumu wakazi waliendeleza shughuli za kawaida.

Ingawa uamuzi huo uliwavunja moyo, wakazi wa eneo hilo waliamua ni lazima maisha yaendelee.

Gavana wa Kisumu Anyang’ Nyong’o aliwashukuru wakazi kudumisha amani akisema ni wakati wa kusonga mbele.

Katika mtaa wa Kondele ambao umekuwa kitovu cha fujo katika eneo hilo, kulikuwa na amani ambayo haijawahi kushuhudiwa.

Shughuli ziliendelea kwa utulivu.

Magari ya uchukuzi wa umma yalifanya kazi kama kawaida.

Mnamo Ijumaa, Amerika ilitoa tahadhari ya usalama kwa raia wake jijini Kisumu kwamba kulikuwa na uwezekano wa kuzuka kwa ghasia baada ya uamuzi wa Mahakama ya Upeo.

  • Tags

You can share this post!

Polisi aua mpenzi wake na kujiua

SHINA LA UHAI: Ukosefu wa visodo tishio kiafya kwa wasichana

T L