• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 8:55 PM
Polisi wawili wafyatuliana risasi wakizozania mwanadada

Polisi wawili wafyatuliana risasi wakizozania mwanadada

Na SAMMY WAWERU

MAAFISA wawili wa polisi wanauguza majeraha mabaya baada ya kufyatuliana risasi Thika Road, Ijumaa jioni.

Duru zinaarifu tukio hilio lilifanyika Quiver Lounge, eneo la Roasters, kwa kile kinadaiwa kuzozania mwanamke.

Kulingana na ripoti ya polisi kutoka kituo cha Kasarani, Nairobi, Festus Musyoka, afisa kutoka Idara ya Upelelezi wa Uhalifu na Jinai (DCI), na Lawrence Muturi wa Kasarani, walifyatuliana risasi Ijumaa, mwendo wa saa tatu na nusu za usiku.

Inasemekana, Muturi ambaye ni konstebo wa kituo cha polisi cha Starehe alifumania mwenzake, Musyoka wa cheo cha konstebo pia, akiwa na mwanamke.

Wawili hao waliishiana kufyatuliana risasi.

Ripoti ya polisi inaarifu, Musyoka ndiye alikuwa wa kwanza kuzua mzozo, ambapo alimpiga mwenzake risasi ya mkono.

“Muturi naye akampiga Musyoka, risasi ya shingo na ambayo ilimfikia mwanamke waliyezozania, Felista Nzisa,” ripoti hiyo inasema.

Musyoka na Felista walikimbizwa katika Hospitali ya Neema Uhai, iliyoko eneo la Ruaraka, Kasarani, naye Muturi akitafuta matibabu Hospital ya Radiant.

Aidha, hali ya Musyoka ilidhoofika, akapelekwa Nairobi Hospital.

Maafisa wa DCI wametwaa silaha walizotumia, huku uchunguzi ukianzishwa.

  • Tags

You can share this post!

Fulham wamwajiri kocha Marco Silva kuwa mrithi wa Scott...

Ni wizi wizi tu!