• Nairobi
  • Last Updated May 20th, 2024 4:32 PM
Rais Ruto na mkewe kusherehekea Krismasi nyumbani Sugoi

Rais Ruto na mkewe kusherehekea Krismasi nyumbani Sugoi

RAIS William Ruto na Mama wa Taifa Rachel Ruto watasherehekea Krismasi leo Jumapili nyumbani kwake Sugoi, Kaunti ya Uasin Gishu.

Kiongozi wa nchi atakuwa akirejea nyumbani na kushiriki hafla ya umma kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe Rais mnamo Agosti 9.

Leo Jumapili atahudhuria ibada ya pamoja ya makamishna mbalimbali katika uwanja wa Eldoret Sports Club.

Ibada hiyo itaongozwa na Kasisi wa Kanisa Katoliki Dayosisi ya Eldoret, Dominic Kimengich, pamoja na viongozi wengine wa kidini kutoka eneo hilo.

Hapo jana Jumamosi, Rais Ruto alikuwa nyumbani akiwapokea wajumbe kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Alitoa pia zawadi ya Krismasi kwa mamia ya wakazi jinsi ambavyo amekuwa akifanya kila msimu wa sherehe hizo na za mwaka mpya.

Seneta wa Uasin Gishu Jackson Mandago na Naibu Gavana John Barorot walisema ibada ya leo Jumapili inatarajiwa kuhudhuriwa na halaiki ya watu.

“Itakuwa hafla ya kwanza ya umma kwa Rais ambaye anatoka kaunti hii na tunatarajia watu wengi wafike,” akasema Bw Mandago.

Mjini Eldoret, jana kulikuwa na hekaheka za hapa na pale, Wakenya wakiabiri magari kuelekea maeneo mbalimbali.

  • Tags

You can share this post!

TUSIJE TUKASAHAU: Bila sare rasmi na beji, ni vigumu raia...

Bei ghali yamaliza ladha ya Krismasi

T L