NA ALEX KALAMA
MSHIRIKISHI wa Pwani Rhoda Onyancha amesema awamu ya pili ya upasuaji wa maiti za wahanga waliofariki dunia baada ya kudaiwa kupotoshwa na wahubiri tata Kaunti ya Kilifi itaanza mnamo Jumatano, Mei 24, 2023.
Akizungumza na wanahabari katika kikuu cha operesheni cha Shakahola ambako ndiko makaburi yamefukuliwa, Bi Onyancha amesema shughuli hiyo itafanyika katika mochari ya hospitali kuu ya kaunti ndogo ya Malindi.
“Operesheni ya kuwatafuta manusura waliokwama msituni inaendelea ile ya kufukua miili tumeisitisha. Hivyo kuanzia kesho Ijumaa wale maafisa waliokuwa wakifanya shughuli ya ufukuaji watapumzika na kupisha wale wataalamu wa upasuaji wa maiti kujitayarisha kwa ajili ya kuanza shughuli hiyo Jumatano,” amesema Bi Onyancha.