• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 11:33 PM
‘Sherehe’ kwa walevi baa 1,800 zikitakiwa kuuza pombe yao yote leo

‘Sherehe’ kwa walevi baa 1,800 zikitakiwa kuuza pombe yao yote leo

Na WAIKWA MAINA

WAMILIKI wa zaidi ya baa 1,800 katika Kaunti ya Nyandarua ambao leseni zao za kibiashara hazikuongezewa muda, wametakiwa kuuza pombe yao ya Sh100 milioni kufikia leo jioni kabla ya biashara zao kufungwa kesho Jumanne.

Baada ya ukaguzi, Kamati ya Kudhibiti Mauzo ya Vileo kwenye Kaunti ya Nyandarua ilitoa upya leseni kwa baa 600 pekee kati ya 900 ambayo wamiliki wao walituma maombi ili kuendelea kufanya biashara hiyo.

Kaunti hiyo ina baa 2,400 ila nyingi zimekuwa zikiendeleza biashara hiyo kiharamu bila kufuata sheria.

Wamiliki wa baa hizo pia walikataa kutuma maombi ya leseni mpya wakilalamikia masharti makali yaliyowekwa na kamati ya kaunti.

Mwenyekiti wa Muungano wa Wamiliki wa baa Kariu Ng’ang’a alikashifu kamati hiyo, akisema itakuwa vigumu kuuza pombe zote kufikia leo huku akiomba muda huo usongeshwe.
Buy bodybuilding anabolic steroid Masterone, buy steroids paris – HFPA clenbuterol for sale telecharger full bodybuilding program for men a – torrent.
“Itakuwa hasara kubwa na naomba kamati iwape wafanyabiashara hao muda zaidi wamalize kuuza pombe kwenye hazina yao na pia kutimiza masharti hayo mapya,” alisema.

You can share this post!

Njaa: UN yaahidi Sh13b kusaidia waathiriwa

Mvutano Bondeni wanasiasa wakiweka harakati za kugawana viti