NA WINNIE ATIENO
KAMPUNI ya kusambaza maji katika Kaunti ya Mombasa, imeanza mikakati mipya ya kusambaza maji kwa mitaa ya wenye mapato ya chini.
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo, Bw Abdirahim Farah, amesema watajitahidi kutatua changamoto sugu ya tangu jadi kuhusu uhaba wa maji maeneo hayo.
“Tutaendelea kushirikiana na wadau wa sekta ya maji ili kukabiliana na changamoto hiyo,” alisema Bw Farah baada ya kukutana na mwenyekiti wa Hazina ya Sekta ya Maji kujadili changamoto zilizopo.