Na ANGELINE OCHIENG
TAHADHARI imetolewa kuhusu kuibuka kwa vifaa ghushi vya kufanyia vipimo vya virusi vya Ukimwi ambavyo vimeingizwa nchini.
Haya yamejiri huku Shirika la Kitaifa la Kudhibiti Ukimwi na Maradhi ya Zinaa (NASCOP) likifichua kuwa idadi ya watu wanaotumia vifaa vya kujipima wenyewe Ukimwi imeongezeka tangu 2018, mpango huo ulipoanzishwa Kenya.
Inahofiwa kuwa watu wengi huenda wanapata vifaa hivyo duni ambavyo havijaidhinishwa kutoka vituo vya kibinafsi vya afya.