NA RUTH MBULA
MAAFISA wa polisi mjini Kisii wamefanikiwa kutwaa magunia mawili ya bangi yenye thamani ya Sh1.5 milioni ambayo ilikuwa ikisafirishwa kwa gari aina ya probox kutoka Igare hadi Keumbu.
Kamanda wa Polisi Kisii Charles Kases bangi hiyo yenye majani yaliyokauka ilikuwa imepakiwa kwenye magunia hayo ya kila 90 kila moja.
Maafisa waliokuwa wakidumisha usalama usiku waliona gari likiwakaribia huku likiendeshwa kwa kasi ya juu.
“Maafisa wetu walianza kulifuata gari hilo aina ya probox ambalo lilitoka kwa barabara kuu na likapata pancha,” amesema Bw Kases.
Ameeleza kwamba walanguzi waliokuwa kwenye gari hilo jeupe walichomoka na wakatimua mbio.
Maafisa walipofanya msako ndani ya gari hilo walipata magunia mawili ya bangi.
Hakuna mshukiwa aliyekamatwa lakini gari la wahalifu hao limepelekwa katika kituo cha polisi cha Kisii Central.
Bangi ambayo watumiaji wengi hukamatwa nayo, mara nyingi huwa imetoka katika taifa jirani la Tanzania na huingizwa nchini kupitia eneo la Kuria.