NA MAUREEN ONGALA
WATOTO watatu waaga dunia huku saba wakilazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kaunti ya Kilifi baada ya kula uyoga wenye sumu; Msimamizi wa Huduma za Matibabu Dkt Malik Tajbhai amethibitisha.
Dkt Tajbhai amesema watoto hao watatu kutoka kijiji cha Katendwa katika wadi ya Bamba walifariki baada ya kula uyoga ambao ni hatari kwa afya ya binadamu mnamo Ijumaa mchana wiki jana.
“Watoto watano wako katika wodi ya kawaida huku wawili wakilazwa katika chumba cha uangalizi wa hali ya juu (HDU),” amesema Dkt Tajbhai.
Bamba iko katika eneobunge la Ganze.