• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 6:55 AM
Wawili wakana kumvua nguo mhasiriwa wa wizi wa mabavu

Wawili wakana kumvua nguo mhasiriwa wa wizi wa mabavu

NA RICHARD MUNGUTI

WASHUKIWA wawili wa wizi wa mabavu waliofumaniwa na mabawabu wakimvua nguo mhasiriwa katika harakati za kumpora wameshtakiwa.

Mohammed Hussein Abdi na Boru Tadicha Guyo walishtakiwa mbele ya hakimu mkazi Mary Njagi kwa wizi wa mabavu.

Abdi na Guyo walikana kwamba walimpora kwa nguvu Job Mutili nguo, na viatu na wakachomoa simu na pesa taslimu Sh5,500 katika mtaa wa mabanda wa Mukuru Kaiyaba jijini Nairobi mnamo Novemba 27, 2022.

Mutili alishambuliwa alipokuwa anarudi nyumbani kutoka kazini mwendo wa saa tatu usiku katika daraja la Kaiyaba.

Polisi walifahamishwa Mutili alivamiwa na kundi la majambazi watatu.

Walimtwanga kwa mawe akaanguka kisha wakaanza kumvua nguo na viatu.

Walinzi katika viwanda vilivyoko katika mtaa huo walimwokoa Mutili kisha wakawatia nguvuni washtakiwa.

Waliwapeleka kituo cha polisi cha South B.

Washtakiwa waliokana shtaka waliomba waachiliwe kwa dhamana.

Hakimu aliwapa dhamana ya Sh200,000 kila mmoja na kutenga kesi isikilizwe Juni 20, 2023.

Itatajwa Januari 23, 2023 washtakiwa waeleze korti ikiwa wamepewa nakala za ushahidi na upande wa mashtaka.

  • Tags

You can share this post!

NGUVU ZA HOJA: Ufala aliouzungumzia Rais Ruto unaweza...

WANDERI KAMAU: Tufufue BBI na kukumbatia mazuri...

T L