• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 9:55 AM
Leba Dei 2023: Viongozi wengi wa kisiasa Pwani wakosa kuhudhuria Sikukuu ya Leba       

Leba Dei 2023: Viongozi wengi wa kisiasa Pwani wakosa kuhudhuria Sikukuu ya Leba      

 

Na WINNIE ATIENO

KAUNTI ya Mombasa imeenda kinyume na kaunti zingine nyingi nchini, baada ya kuandaa sherehe za kuadhimisha siku ya kimataifa ya Leba Dei.

Mbali na Kaunti ya Nairobi ambapo sherehe za kitaifa ziliandaliwa, kaunti nyingi ikiwemo tano zilizo Pwani hazikuandaa hafla yoyote.

Katika Kaunti ya Mombasa, mashirika mbalimbali ya serikali ya kitaifa pamoja na serikali ya kaunti yalijumuika kusherehekea juhudi za wafanyakazi kujenga taifa, katika uwanja wa Tononoka.

Hata hivyo, sherehe hizo zilizoandaliwa katika uwanja wa Tononoka hazikuhudhuriwa na viongozi wengi wa kisiasa.

Akiwakilisha serikali ya kaunti katika maadhimisho hayo, Waziri wa Utumishi wa Umma, Vijana, Jinsia na Michezo katika kaunti, Bw Kenneth Muigai, alitilia mkazo hitaji la waajiri wote kulipa wafanyakazi mishahara kwa wakati unaofaa.

Kwa upande mwingine, Naibu Kamishna wa Kaunti, Bw Ronald Mwiwawi, alitoa changamoto kwa wawekezaji kubuni nafasi zaidi za ajira kama njia mojawapo ya kukabiliana na uhalifu.

 

  • Tags

You can share this post!

Ajabu watu 2 pekee wakihudhuria sherehe ya Leba Dei Eldoret...

Atwoli amtaka Raila kusitisha maandamano

T L