NA MWANGI MUIRURI
MWANAMKE ameteketea na kubaki majivu baada ya petroli, mitungi ya gesi na bidhaa nyingine kulipuka na kusababisha moto mkubwa Murang’a.
Mkuu wa polisi Kahuro, Catherine Ringera, amethibitisha kutokea kwa mkasa huo wa saa kumi na moja Ijumaa jioni katika kituo cha kibiashara cha Mugeka huku akisema uchunguzi umeanzishwa.
Aliyefariki ametambuliwa kuwa ni Joyce Mureithi.
Wakazi, zimamoto na maafisa wa polisi wameonekana katika eneo hilo katika harakati za uokozi.