• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 12:18 PM
Mwanamke ateketea na kubaki majivu katika mkasa wa moto Murang’a

Mwanamke ateketea na kubaki majivu katika mkasa wa moto Murang’a

NA MWANGI MUIRURI

MWANAMKE ameteketea na kubaki majivu baada ya petroli, mitungi ya gesi na bidhaa nyingine kulipuka na kusababisha moto mkubwa Murang’a.

Mkuu wa polisi Kahuro, Catherine Ringera, amethibitisha kutokea kwa mkasa huo wa saa kumi na moja Ijumaa jioni katika kituo cha kibiashara cha Mugeka huku akisema uchunguzi umeanzishwa.

Aliyefariki ametambuliwa kuwa ni Joyce Mureithi.

Wakazi, zimamoto na maafisa wa polisi wameonekana katika eneo hilo katika harakati za uokozi.

  • Tags

You can share this post!

Rotich atabasamu DPP akikataa kuhoji mashahidi kesi ya Sh63...

Mke wa MCA Trans Nzoia alivyotapeliwa nusu milioni akisaka...

T L