• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 2:24 PM
Polisi wamsaka mwanamume anayedaiwa kumuua mke, mtoto kijijini Kodwar B

Polisi wamsaka mwanamume anayedaiwa kumuua mke, mtoto kijijini Kodwar B

NA GEORGE ODIWUOR

POLISI wa Rachuonyo Mashariki wanamtafuta mwanamume ambaye anadaiwa kuua mwanamke na mtoto wake wa umri wa miaka miwili.

Kisa hicho kimetokea leo Ijumaa, zikiwa ni wiki mbili tu tangu mwanamke huyo aanze kuishi na mwanamume huyo katika kile kinachorejelewa kama mume na mke.

Mshukiwa mwenye umri wa miaka 32 yuko mafichoni.

Mwanamke aliyetambuliwa kama Mitchel Awuoro alikatwa shingoni.

Naye mtoto wake alipigwa usoni hadi akaaga dunia. Pia mtoto huyo alikuwa na jeraha shingoni.

Miili yao ilipatikana kwenye godoro walilolalia likiwa limeloa damu katika nyumba yao kijijini Kodwar B, lokesheni ya Kodumo Mashariki.

Mamamkwe wa mwanamke huyo ndiye alipata miili hiyo baada ya marehemu kukosa kupokea simu mara kadhaa.

Naibu chifu wa eneo hilo Bw Denis Abongo amesema mshukiwa ni kibarua anayefanya kazi mjini Sondu.

Hata hivyo, amesema wanandoa hao hawakuonyesha dalili zozote za kutofautiana kabla ya kutokea kwa mauaji hayo.

“Wanandoa hao walikula chajio pamoja kabla ya kuenda kulala. Mamamkwe wa marehemu amesema hakuona dalili zozote za mvutano baina ya wawili hao,” Bw Abongo amesema.

Ameongeza: “Mamake mshukiwa alienda kubisha mlango lakini hakuna aliyejibu. Alipoamua kujitoma ndani ya nyumba alipata miili ya mwanamke na mtoto wake.”

Kamanda wa Polisi Homa Bay Samson Kinne amesema maafisa wanaendesha uchunguzi.

“Maafisa wa upelelezi wanachunguza kisa hicho,” akasema kamanda Kinne akiongeza kuwa mwanamume huyo ambaye yuko mafichoni ndiye mshukiwa mkuu na akikamatwa atahojiwa

Miili hiyo imepelekwa katika mochari ya hospitali ya kaunti ndogo ya Rachuonyo Kusini.

  • Tags

You can share this post!

Wahisani waombwa kujitokeza kusaidia shule ya watoto viziwi...

Diana Marua ashambulia mwalimu wake aliyewahi kumwambia...

T L