• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:50 AM
Diana Marua ashambulia mwalimu wake aliyewahi kumwambia ‘hatafika mbali’

Diana Marua ashambulia mwalimu wake aliyewahi kumwambia ‘hatafika mbali’

NA MERCY KOSKEI

Mwanakontenti wa You Tube Diana Marua amewaacha wanamitandao kwa mshangao baada ya kumkosoa mwalimu wake wa zamani wa somo la hesabu kwa unyanyasaji aliyovumilia akiwa shuleni.

Kupitia mtandao wake wa Instagram, Bi Marua alichapisha video, Octoba 5, 2023 akikumbuka jinsi mwalimu wake wa hesabu alivyomfedhehesha na kumdharau, akisema kuwa alimchukulia kama mtu asiyefaa chochote maishani.

Hata hivyo, Bi Marua alichukua fursa hiyo kuonyesha baadhi ya mali anayomiliki licha ya mwalimu wake kusema kuwa hatafanikiwa.

Kupitia video hiyo, Bi  Marua alionyesha gari lake na jumba la kifahari kama ushuhuda wa mafanikio yake, licha ya dhihaka na unyanyasaji aliopata kutoka kwa mwalimu wake.

Kwa kifahari, alifichua kuwa kwa sasa ameajiri watu wengi, huku akionyesha sebule yake, akiashiria kama jibu kwa waliotilia shaka maisha yake ya baadaye.

Katika video hiyo, mwanakontenti huyo alizungumzia childhood trauma na kueleza azma yake ya kuthibitisha kuwa mwalimu wake wa hisabati alikosea kumkashifu.

“Nataka taarifa hii iwafikie … [tunabana majina yao kwa sababu za kisheria] walionidhalilisha nikiwa shuleni. Gari hii aina ya Mercedes Benz ni moja tu kati ya magari mengi ninayomiliki. Jumba hili la kifahari pia ni langu. Ifikie mwalimu wangu wa hesabu,” alisema Bi Marua.

Bi Marua aliendelea kwa kuonyesha vyakula ambavyo vilikua kwenye friji kabla ya kupanda juu na kuonyesha nyumba yake ya ghorofa.

“Unajua huyu mwalimu alinifanyia nini, inaniuma kukumbuka. Leo mimi ni mwajiri. Hawa ni wafanyakazi wangu. Mwalimu huyo alidhani nitakuwa masikini milele. Alidhani nitalala njaa lakini Mungu amenisaidia,” aliongeza.

  • Tags

You can share this post!

Polisi wamsaka mwanamume anayedaiwa kumuua mke, mtoto...

Kunguni: Algeria yapiga dawa kwa vyombo vya usafiri vya...

T L