• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 8:55 PM
Tanzia: Nyamira yapoteza MCA kupitia ajali ya barabara

Tanzia: Nyamira yapoteza MCA kupitia ajali ya barabara

NA SAMMY WAWERU

KAUNTI ya Nyamira inaomboleza kifo cha diwani (MCA) wa Wadi ya Nyamaiya, aliyefariki Jumatatu, Agosti 7, 2023 katika ajali mbaya ya barabara.

Bw Elijah Osiemo alikumbana na mauti gari alimokuwa lilipohusika kwenye ajali katika barabara ya Maai Mahiu – Naivasha.

MCA wenza, Duke Masira na Priscilla waliosafiri pamoja waliuguza majeraha na wanaendelea kupata matibabu katika Hospitali ya Naivasha Level Four.

“Kaunti imepoteza kiongozi mwenye bidii, talanta, maono na aliyekuwa na mchango mkubwa katika uongozi na kisiasa,” Gavana wa Nyamira, Amos Nyaribo akamuomboleza kupitia taarifa kwa vyombo vya habari

Bw Nyaribo aidha ameagiza mwili wa mwendazake kusafirishwa hadi Nairobi kuhifadhiwa.

“Kwa madiwani wanaouguza majeraha, ninawatakia afueni ya haraka,” Bw Nyaribo akasema, akituma rambirambi kwa familia, jamaa na marafiki wa MCA Osiemo.

Bw Osiemo pia alikuwa kiongozi wa wengi Bunge la Kaunti ya Nyamira.

  • Tags

You can share this post!

Korti yaita maafisa 2 wa polisi kujibu madai ya kukarabati...

Babu Owino: Ruto anazima ndoto za wanafunzi kukata kiu cha...

T L