• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 10:50 AM
Bolt yamfuta kazi dereva aliyefungua zipu kimakusudi na kuwashtua wateja

Bolt yamfuta kazi dereva aliyefungua zipu kimakusudi na kuwashtua wateja

NA MERCY KOSKEI

KAMPUNI ya uchukuzi ya teksi inayomiliki apu maarufu ya Bolt imemwachisha kazi dereva aliyesajiliwa chini yao, baada ya kunaswa na kamera akionyesha uchi wake kwa wateja wa kike walioabiri gari lake.

Video hiyo ya kuchukiza ilisambazwa na aliyekuwa Gavana wa Nairobi Mike Sonko katika ukurasa wa akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa X (zamani Twitter), imeonyesha dereva huyo akifungua zipu ya suruali kabla ya kuonyesha uchi wake.

Jambo hilo liliwakera abiria hao kiasi cha kuamuru dereva huyo kusimamisha gari na kuwashusha kabla ya kufika walipokuwa wanaelekea.

“Kwa nini unavua nguo? Nishukishe hapo. Sally! Shuka, mwanamume huyu yuko uchi,” abiria huyo alisikika akimweleza mwanzake kwenye video hiyo ambayo imeibua gumzo mitandaoni.

Katika taarifa yake, Bolt wamefichua kuwa wamechukua hatua za kinidhamu dhidi ya dereva huyo aliyenaswa, na kumpiga marufuku kutoa huduma zozote kwenye jukwaa lao.

Kampuni hiyo imejutia tukio hilo, ikieleza kuwa wanathamini usalama wa wateja wao wakati wote na kuongeza kuwa hawatavumilia tabia mbovu kutoka kwa madereva wakatili.

“Tunashirikiana kikamilifu na waathiriwa. Kama Bolt, usalama wa madereva na abiria wetu unasalia kuwa kipaumbele. Tunajitolea kwa umakini na tunasaka majibu ya haraka katika kushughulikia matukio kama haya,” Bolt imesema kwenye taarifa yake.

  • Tags

You can share this post!

Mwangaza asubiri kikao cha bunge la kaunti kupata mwanga...

Sonko alipa dhamana kumsaidia ‘wakili feki’...

T L