• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:50 AM
Ichung’wah ashtakiwa na wakili Omari kwa matusi

Ichung’wah ashtakiwa na wakili Omari kwa matusi

Na RICHARD MUNGUTI

KIONGOZI wa wengi katika bunge la kitaifa aliyepia mbunge wa Kikuyu, Kimani Ichung’wah ameshtakiwa na wakili kwa madai alimtusi na kudumisha hadhi 

Sasa wakili Danstan Omari anaomba mahakama kuu imwamuru Bw Ichung’wah amlipe fidia ya Sh11 milioni kwa kushusha hadhi yake.

Bw Omari ameeleza katika kesi hiyo kwamba mwanasiasa huyo alichapisha katika mtandao wake wa twiter madai kwamba yeye (Omari) amekuwa akionekana katika barabara ya Koinange Nairobi inayohusishwa na ukahaba.

Wakili huyo amesema Bw Ichung’wah alituma ujumbe huo kwa Twitter punde tu alipomaliza mahojiano na kituo cha televisheni cha NTV mnamo Feburuari 1, 2023.

Baada ya mahojiano, kituo cha NTV KENYA kilipeperusha habari kikimnukuu Bw Omari akisema “Rais mstaafu Uhuru Kenyatta na Raila Odinga ni viongozi mashuhuri wa kimataifa sio kama Rais Ruto na watu wengine kama Ichung’wah anayejulikana tu eneo la uwakilishi bunge la Kikuyu.”

Akimjibu Bw Ichung’wah aliandika maneno haya katika mtandao wake wa twitter @KIMANIICHUNG’WAH, “Phew, angalau ninajulikana Kikuyu na watu wangu sio kama wakili mdanganyifu anayejulikana tu katika barabara ya Koinange.”

Kutokana na maneno hayo Bw Omari amesema amechukuliwa kuwa mtu asiyemwadilifu ikikumbukwa kuwa ameoa na yuko na watoto.

Amesema maneno hayo yametishia ndoa yake.

Anaomba mahakama kuu imzuie Bw Ichung’wah kutochapisha tena maneno hayo ya kuudhi.

Mahakama pia imeombwa imwamuru Bw Ichung’wah amwombe msamaha mbali na kumwamuru amlipe fidia ya Sh11 milioni.

  • Tags

You can share this post!

Ogolla apandishwa cheo kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, CDF

Polisi aliyepora wafanyabiashara Sh2.8 milioni ashtakiwa

T L