• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:57 PM
KRA yapata Kamishna Mkuu mpya

KRA yapata Kamishna Mkuu mpya

NA CHARLES WASONGA

WAZIRI wa Fedha Profesa Njuguna Ndung’u amemteua Humphrey Wattanga Mulongo kuwa Kamishna Mkuu mpya wa Mamlaka ya Ukusanyaji Ushuru Nchini (KRA).

Kwenye tangazo katika gazeti rasmi la serikali toleo la Agosti 22, 2023, Profesa Ndung’u amesema kuwa Bw Wattanga atahudumu kwa kipindi cha miaka mitatu.

Bw Wattanga anachukua nafasi ya James Githii Mburu ambaye alijiuzulu mnamo Februari 2023 baada ya kuhudumu kwa miaka mitatu na miezi saba.

Tangu kujiuzulu kwa Bw Mburu, Rispah Simiyu amekuwa akihudumu kama Kaimu Kamishna Mkuu wa KRA.

Bi Simiyu ni Kamishna wa KRA anayesimamia Idara ya Ushuru unaokusanywa kutoka humu nchini.

Mwenyekiti wa Bodi ya KRA Anthony Mwaura alisema kuwa Bw Mburu aliondoka mnamo Februari 23 ili apate nafasi ya kushughulikia shughuli zake za kibinafsi.

Hapo awali, Bw Wattanga aliwahi kuhudumu kama mwanachama wa Tume ya Ugavi wa Mapato (CRA) kwa muda wa miaka sita, baada ya kuteuliwa na Rais mstaafu Uhuru Kenyatta mnamo 2016.

  • Tags

You can share this post!

Mshukiwa wa mauaji ya afisa wa DCI naye auawa kwa risasi

Mshauri wa kijasusi wa gavana alikufa kwa kula sumu –...

T L