• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 6:50 AM
Lusaka asifu uongozi wa wanawake

Lusaka asifu uongozi wa wanawake

Na BRIAN OJAMAA

SPIKA wa Bunge la Seneti Ken Lusaka amewataka wanawake kote nchini wajitokeze kuwania nafasi za uongozi ili hitaji la kikatiba la usawa wa jinsia liafikiwe.

Bw Lusaka alisema wanawake ambao wapo uongozi kwa sasa wameonyesha sifa nzuri na kuwatumikia vyema, ndiposa wengine wanafaa wajitokeze zaidi kushindania viti vya uongozi 2022.

Kiongozi huyo ambaye anamezea mate kiti cha ugavana wa Kaunti ya Bungoma mnamo 2022, alikuwa akizungumza kwenye afisi za Naibu Kamishina zinazoptaikana eneo la Kamukuywa wakati wa kutawazwa kwa mama Lorna Wanyonyi Mumelo kama chifu mpya wa Lokesheni ya Kamukuywa.

“Tuwaunge mkono wanawake wetu kwa sababu majukumu yale yanatekelezwa na wanaume pia yanaweza kutekelezwa na wanawake hata vyema zaidi,” akasema.

You can share this post!

Wito wakazi wachague wanasiasa waadilifu

Ngamia, mnyama ambaye manufaa yake hayakadiriki

T L