• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 4:42 PM
Ruto awapongeza wanajeshi wa KDF kwa kulinda nchi dhidi ya adui

Ruto awapongeza wanajeshi wa KDF kwa kulinda nchi dhidi ya adui

NA WINNIE ONYANDO

RAIS William Ruto mnamo Jumamosi amewapongeza wanajeshi wa Kenya (KDF) kwa kujitolea kwao kulinda taifa.

Rais alikuwa akizungumza wakati wa kuzinduliwa kwa mnara wa kumbukumbu ya wanajeshi waliofariki vitani.

Sherehe hizo zilifanyika Embakasi Garrison, Nairobi.

Katika hotuba yake, Rais Ruto alisisitiza jukumu muhimu ambalo KDF inatekeleza katika kudumisha amani na usalama, ndani na nje ya mipaka ya nchi.

“Ninasimama hapa kuwashukuru kwa juhudi mnazoweka kwa niaba yetu. Mara nyingi, si rahisi kamwe, lakini mnatoka na kutekeleza wajibu wenu kwa ujasiri,” akasema Rais Ruto.

Rais Ruto alitangaza kuwa KDF itafaidika na mpango wa ujenzi wa nyumba za bei nafuu kama ishara ya kuonyesha shukrani kwa huduma yao ya kujitolea.

Rais Ruto pia alifichua kukamilika kwa mchakato wa ujenzi wa nyumba 9,000 za wafanyikazi wa KDF.

Rais alisisitiza kuwa serikali yake itaendelea kusimama na wanajeshi hao na kuboresha mazingira yao ya kufanyia kazi.

  • Tags

You can share this post!

CDF Francis Ogolla amuomba Rais Ruto msamaha kwa kusahau...

Nyakati ngumu makundi mengi yakishindwa kulipa mikopo ya...

T L