NA ERIC MATARA
WATU sita wamejeruhiwa alfajiri wakiingia katika uwanja wa Kericho Green kwa sherehe za sikukuu ya Mashujaa.
Mtoto ni miongoni mwa sita hao waliojeruhiwa katika mkanyagano uliotokea katika Lango C la kuingia katika uwanja huo.
Naye mwanahabari Vitalis Kimutai wa shirika la Nation Media Group (NMG) linalomiliki Taifa Leo amepoteza simu yake.
“Ni kweli nimepoteza simu yangu nikiingia uwanjani,” amesema mwanahabari wetu Kimutai.
Makala ya mwaka huu 2023 ni ya 60.
Awali sherehe hiyo ilifahamika kama ‘Kenyatta Dei’.