• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 10:50 AM
Watu sita wapelekwa hospitalini baada ya kujeruhiwa wakiingia uwanjani Kericho Green

Watu sita wapelekwa hospitalini baada ya kujeruhiwa wakiingia uwanjani Kericho Green

NA ERIC MATARA

WATU sita wamejeruhiwa alfajiri wakiingia katika uwanja wa Kericho Green kwa sherehe za sikukuu ya Mashujaa. 

Mtoto ni miongoni mwa sita hao waliojeruhiwa katika mkanyagano uliotokea katika Lango C la kuingia katika uwanja huo.

Naye mwanahabari Vitalis Kimutai wa shirika la Nation Media Group (NMG) linalomiliki Taifa Leo amepoteza simu yake.

“Ni kweli nimepoteza simu yangu nikiingia uwanjani,” amesema mwanahabari wetu Kimutai.

Makala ya mwaka huu 2023 ni ya 60.

Awali sherehe hiyo ilifahamika kama ‘Kenyatta Dei’.

  • Tags

You can share this post!

Serikali yaambia wakulima waridhike na bei ya Sh4,000 kwa...

Wabunge wa Azimio kususia vikao hadi Sabina avuliwe wadhifa...

T L