• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 4:54 PM
Ghana kuwapiga faini wanaosafiri huko bila vyeti

Ghana kuwapiga faini wanaosafiri huko bila vyeti

Na MASHIRIKA

ACCRA, GHANA

GHANA imesema itayapiga mashirika ya ndege faini ya Sh350,000 kwa kila abiria anayeingia nchini humo bila cheti cha chanjo ya Covid-19.

Chini ya masharti hayo ambayo yanaanza kutekelezwa leo Jumatano, mashirika hayo pia yatapigwa faini ikiwa abiria hawatakuwa wamejaza fomu maalum ambayo imetolewa na wizara ya afya nchini humo.

Ijapokuwa raia wa taifa hilo ambao wataingia humo bila kutimiza kanuni hizo watawekwa karantini kwa siki 14, raia wa kigeni watakuwa hatarini kuzuiwa kuingia nchini humo.

Ghana ni miongoni mwa nchi ambazo zimeanza kuchukua tahadhari kudhibiti maambukizi ya virusi vya corona, baada ya virusi aina ya Omicron kugunduliwa nchini Afrika Kusini mnamo Novemba.

You can share this post!

Wito watu wapime kansa ili kupunguza ada za kutibu

Mwanamuziki Koffi Olomide ahukumiwa kwa kupatikana na hatia...

T L