• Nairobi
  • Last Updated May 11th, 2024 7:55 AM
Jinsi Rais Joe Biden alivyonusurika gari lilipogonga msafara wake

Jinsi Rais Joe Biden alivyonusurika gari lilipogonga msafara wake

NA MASHIRIKA

WASHINGTON, MAREKANI

RAIS wa Marekani Joe Biden alipelekwa upesi eneo salama baada ya gari moja nje ya safari ya kiongozi huyo kugonga gari moja kwenye msafara wa kiongozi huyo mnamo Jumapili usiku.

Biden na mkewe Jill Biden walikuwa wanatoka makao makuu ya sekretarieti ya kampeni yake na makamu wa rais Khamala Haris wakati ajali hiyo ilitokea.

Wote walikuwa salama, kwa mujibu wa maafisa wa serikali.

Biden na mkewe walikuwa wanatoka makao makuu ya kampeni ya Biden-Harris 2024 katika jiji la Wilmington saa mbili za usiku baada ya kupata chajio na wanachama wa timu inayompangia mikakati ya kupiga kampeni kutetea urais, Ikulu ya White House imesema.

Baadaye kiongozi huyo wa taifa hilo lenye ushawishi mkubwa aliendelea na safari yake bila tatizo lolote.

  • Tags

You can share this post!

KWPL kuchukua mapumziko mafupi warembo wapunge unyunyu...

Wanaume wa kupenda ndogondogo watiwa majaribuni kwa...

T L