• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 12:38 PM
Mwanawe Rais wa Somalia atoroka Uturuki baada ya kuua bodaboda

Mwanawe Rais wa Somalia atoroka Uturuki baada ya kuua bodaboda

Na MASHIRIKA

MWANA wa kiume wa Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud, Mohammed Hassan Sheikh Mohamud, aliyedaiwa kugonga na kumuua mwendeshaji pikipiki jijini hapa ametoroka Uturuki.

Hii ni licha ya ilani ya kutolewa kwamba akamatwe akionekana popote ulimwenguni, vyombo vya habari vimesema.

Polisi walikuwa wamemwachilia huru Mohammed Hassan Sheikh Mohamud bila dhamana baada ya uchunguzi kuhusu kisa hicho kufanywa, lilisema gazeti la Cumhuriyet.

“Mshukiwa ameondoka Uturuki bila vikwazo vyovyote,” akasema meya wa Instanbul Ekrem Imamoglu.

Soma pia: https://taifaleo.nation.co.ke/habari-mseto/mwanawe-rais-atupwa-rumande-baada-ya-kukanyaga-mtu-barabarani

  • Tags

You can share this post!

Kesi ya Muingereza anayedaiwa kupiga dafrao na kuua mkewe...

Chelsea, Arsenal na Man-Utd ni vichapo tu!

T L