NA MASHIRIKA
DAR ES SALAM, TANZANIA
MAMLAKA ya safari za ndege nchini Tanzania (TCAA) imekana madai kuwa iliruhusu ulanguzi wa wanyamapori kutoka mbuga moja hadi mataifa ya Mashariki ya Kati.
Hii inafuatia madai kwenye mitandao ya kijamii kwamba wanyamapori wanasafirishwa kwa ndege za mizigo kutoka Loliondo, karibu na mbuga maarufu ya kitaifa ya Serengeti hadi kwa Muungano wa Milki za Kiarabu (UAE).
Lakini TCAA imetaja madai hayo kama “ya uongo” ikisema uwanja wa ndege wa Loliondo si kituo cha kuingia na kuondoka nchini Tanzania.