• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:57 PM
TANZIA: Colin Powell afariki

TANZIA: Colin Powell afariki

Na AFP

WASHINGTON, Amerika

MWEUSI wa kwanza kabisa kuwahi kuwa Waziri wa Masuala ya Kigeni wa Amerika, Colin Powell alifariki Jumatatu kutokana na kile kilichotajwa kama changamoto za Covid-19.

Kulingana na taarifa kutoka kwa familia yake iliyotumwa kupitia mtandao wa Facebook, Powell aliyekuwa na umri wa miaka 84, alikuwa amepewa chanjo.

“Tumempoteza mume mzuri, baba na babu,” familia yake ikisema.

Poweli ndiye mtu mashuhuri wa hivi punde kufariki kutokana na ugonjwa wa Covid-19 ambao umesababisha maafa makubwa kando na kuvuruga chumi za mataifa ya ulimwengu kwa ujumla.

Marehemu anakumbukwa kwa kuongoza vita vya Ghuba mnamo mwaka wa 1991. Vita hivyo, vilimpa Powell umaarufu mkubwa kiasi kwamba wakati mmoja alidhaniwa angefaulu kuchaguliwa Rais wa kwanza mweusi Amerika.

Hata hivyo, miaka ya baadaye alitupilia mbali wazo la kuwania urais, akatofautiana na chama chake cha Republican na kuunga mkono azma ya Barack Obama.

Powell alizaliwa mnamo Aprili 5, 1937 katika mji wa Harlem.

Alilelewa na kusoma jijini New York hadi akapata shahada katika taalamu ya sayansi ya ardhini (Geology).

Alihudumu katika jeshi la Amerika na kupanda cheo hadi kuwa Luteni Jenerali. Aliwahi kuhudumu katika mataifa kama vile Ujerumani, Vietnam, miongoni mwa mengine.

Tafsiri: CHARLES WASONGA

You can share this post!

‘Kenya imefanikiwa kuwakabili kikamilifu nzige...

Maswali Ruto akiidhinisha wawaniaji ugavana Pwani

T L