• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 10:50 AM
‘Kenya imefanikiwa kuwakabili kikamilifu nzige waharibifu’

‘Kenya imefanikiwa kuwakabili kikamilifu nzige waharibifu’

Na SAMMY WAWERU

KENYA imefanikiwa kukabili kikamilifu nzige waharibifu, serikali imetangaza.

Tangazo hili limejiri miaka miwili baada ya Kenya hasa maeneo kame kuvamiwa na nzige, 2019 na 2020.

Katibu katika Wizara ya Kilimo, Mifugo na Samaki Prof Boga Hamadi alisema wadudu hao wamekabiliwa chini ya athari haba kwa mimea, malisho ya mifugo na kwa mazingira.

Akizungumza jijini Nairobi, Prof. Boga alisema hatua hiyo imefanikishwa kwa ushirikiano wa karibu na Shirika la Chakula na Kilimo (FAO-UN) na Benki Kuu ya Dunia.

“Ninathibitisha kuwa Kenya sasa ni salama, haina nzige,” katibu akaambia Taifa Leo kupitia mahojiano katika Kilimo House, Nairobi.

Hata hivyo, alidokeza kwamba nchi jirani ya Somalia na Ethiopia baadhi ya maeneo yamethibitishwa kuvamiwa na nzige.

“Tupo makini kama taifa wadudu hao wasirejee,” Prof Boga akaahidi.

“FAO kwa ushirikiano na Benki Kuu ya Dunia inaendelea kutoa msaada kukabili wadudu hao Somalia na Ethiopia,” akasema.

Zaidi ya kaunti 32 zilikumbwa na nzige hao waharibifu, ambao walivamia mimea na malisho ya mifugo.

You can share this post!

ONYANGO: Mchujo ufanywe siku moja kubana nje wanaorukaruka

TANZIA: Colin Powell afariki

T L