• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 10:50 AM
Ukraine yalalama Urusi inaua na kuzika maelfu ya raia wake

Ukraine yalalama Urusi inaua na kuzika maelfu ya raia wake

NA MASHIRIKA

KYIV, UKRAINE

WANAJESHI wa Urusi wanaaminika kuua maelfu ya raia wa Ukraine mjini Mariupol na kuwazika katika kaburi la halaiki.

Serikali ya Ukraine ilidai Ijumaa kuwa, watu wanaouawa wanazikwa kwenye kaburi la pamoja la kina cha urefu wa mita 30 (futi 98) karibu na kijiji cha Manhush, magharibi mwa jiji la Azov.

Ukraine ilisema kuwa imepata picha za setelaiti zilizopigwa kutoka angani zinazoonyesha makaburi hayo ya halaiki.

Kampuni ya teknolojia ya Amerika, Maxar pia ilidai kwamba, picha zake za satelaiti zilizopigwa hivi majuzi zinaonyesha kuwepo kwa makaburi mapya ya halaiki katika ukingo wa kaskazini-magharibi mwa Manhush, Ukraine.

“Picha tulizo nazo za satelaiti zilizonaswa kati ya Machi na Aprili zinaonyesha matuta makubwa yanayoaminika kuwa makaburi yaliyozikwa watu kati ya Machi 23-26, mwaka huu. Picha zetu zinaonyesha kuwa eneo hilo lina zaidi ya makaburi zaidi ya 200,” ikasema kampuni ya Maxar.

Kampuni hiyo ya Amerika pia imechapisha msururu wa picha za satelaiti zinazodaiwa kuonyesha eneo la kaburi la watu wengi karibu na Mariupol.

  • Tags

You can share this post!

Jimmy: Jaramogi alimsaidia sana Kibaki kuingia siasa

Wanyonyi anyimwa tikiti kuwania ugavana Nairobi

T L