Na MARGARET MAINA
VIDONDA vya tumbo ni tatizo linalotokea baada ya kuta za tumbo au utumbo mdogo kuwa na vidonda.
Hali hii hutokea baada ya kuharibika kwa ukuta wenye ute unaozuia kemikali za kuyeyusha chakula.
Kemikali ambayo ni asidi inayozalishwa mwilini kiasili husaidia kuyeyusha chakula na kuua wadudu tumboni na kama ukuta wenye ute utaharibiwa na kushindwa kufanya kazi, basi hiyo kemikali (asidi) itaathiri tumbo au utumbo na kuruhusu bakteria kuendelea kusababisha vidonda vya tumbo.
Vidonda vya tumbo vinatibika kirahisi ila vikicheleweshwa bila kutibiwa huweza kusababisha tatizo kubwa.
Ni tatizo linalotesa sana na kuwanyima raha watu wengi. Pia husababisha magonjwa mengine kama kansa, amoeba (amiba), homa na kupungua uzani.
Chanzo cha vidonda vya tumbo
Vidonda vya tumbo vina vyanzo tofauti ili vyote ni vile vinavyohusiana na mmeng’enyo. Vyanzo hivyo ni;
Dalili za vidonda vya tumbo
Dalili za vidonda vya tumbo hujitokeza baada ya kula au kabla ya kula, ila mara nyingi wengi huwa wanazipuuza na kuendelea kukuza tatizo. Vidonda vya tumbo vina dalili kama:
Cha kufanya ili kuepukana na vidonda vya tumbo
Maumivu yakizidi, pata ushauri wa daktari.