• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 11:33 PM
Akothee atishia kuzua fujo kwenye benki baada ya pesa zake kutolewa kwa ATM bila idhini   

Akothee atishia kuzua fujo kwenye benki baada ya pesa zake kutolewa kwa ATM bila idhini  

NA MERCY KOSKEI

MWANAMUZIKI tajika Esther Akoth maarufu kwa jina la jukwaani kama Akothee, amefichua kuwa alipoteza kiasi kikubwa cha pesa kwa njia tatanishi kutoka kwa akaunti yake ya benki.

Kupitia mtandao wake wa kijamii wa Facebook, Octoba 7, 2023, mama huyo wa watoto watano alifichua kuwa mtu asiyejulikana alipata maelezo ya akaunti yake na kuishia kutoa pesa kwa kutumia ATM.

Hata hivyo, bila kutaja benki hiyo, Akothee aliwaacha wengi na maswali jinsi mtu anaweza kutoa pesa bila ya yeye na benki kujua.

Kupitia chapisho hilo, Akothee alifichua kuwa haikuwa mara yake ya kwanza kupata matatizo na benki hiyo, kwani akaunti yake ilidukuliwa mapema mwaka huu.

“Kesi ya pili ilitokea Septemba 12, kiasi kikubwa cha pesa kilitolewa kwenye akaunti yangu kwa kutumia ATM ilhali mimi binafsi sijawahi kutoa zaidi ya Sh30, 000 kwa ATM. Nikihitaji zaidi ya Sh30, 000, nitalazimika kupiga simu benki ili waongeze kiwango cha pesa,” alifoka.

Mwimbaji huyo mwenye umri wa miaka 43 alitishia kufanya chochote, ikiwa ni pamoja na kusababisha vioja kwenye benki hiyo ili warejeshe pesa zake.

“Watahisi uwepo wangu katika makao yao makuu siku ya Jumatatu, sina uhusiano wowote na mtu ikifika ni pesa zangu, nitaenda huko na timu yangu kuchukua pesa, kama ni vita tupo tayari.

“Sina mfadhili anayenitumia pesa, nafanya kazi. Kwa sasa, niruhusu niende kujivinjari baada ya kufanya kazi wiki nzima. Ninataka pesa zangu zirudi kwenye akaunti yangu kufikia Jumatatu,” alisema.

 

 

 

  • Tags

You can share this post!

Letoo ‘amteua’ aliyekuwa mume wa Akothee kuwa...

Mhubiri Ng’ang’a ashangaza kwa kukataa sadaka ya Sh500

T L