• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 8:55 PM
Ambia Samidoh akujengee boma lako, Karen Nyamu aambiwa

Ambia Samidoh akujengee boma lako, Karen Nyamu aambiwa

NA FRIDAH OKACHI

WATOAJI maoni na wajuaji mtandaoni sasa wanamtaka Seneta Maalum Karen Nyamu amuombe mwanamuziki Samuel Muchoki almaarufu ‘Samidoh’ amjengee boma lake. 

Cheche hizi zinarushwa baada ya Bi Nyamu kupakia video moja akiwa kwenye boma ambalo mtandaoni linarejelewa kama la ‘mke mwenza’.

Video hiyo kwenye akaunti yake ya Facebook na Instagram iliyoonyesha wanawe wakisherekea siku ya Krismasi huko Nyandarua kwa mwanamuziki Samidoh, ilizua maoni mbalimbali na mseto.

Wapo mashabiki waliosema ni kinyume na tamaduni za Wakikuyu.

Video hiyo ilionyesha watoto na mwanamuziki huyo wakilisha kuku na bata. Bi Nyamu akirekodi matukio hayo kwa furaha.

“Vile watoto wanafurahia mazingira ya mashambani itabidi turefushe msimu wa Krismasi!” aliandika Bi Nyamu.

Video iliyochapishwa Desemba 26, 2026, na mwanasiasa huyo, ilifanya mashabiki kumiminika kwenye ukurasa huo na kuchangia. Walitaka kufahamu inakuwaje anafurahia kuingia nyumba ya ‘mke mwenza’ na kulala humo.

“Yaani uko sawa? Kwa boma la mwanamke mwingine… Kitakuramba… siku yako itafika,” akaandika Grace Wanjiku.

Katika kuchangia kwa video hizo, seneta huyo na mashabiki walianza kujibizana kuhusiana na mwaliko alioupata kufika Ol Joro Orok ambapo ni kijiji cha kwa kina Samidoh.

“Seneta mzima ulishindwa kujengewa kwako…,” alisema Everlyne Muteti.

Bi Nyamu alimjibu hivi: “Everlyne Muteti ungeongeza mscheeewww hiyo machungu iingie vizuri (sic).”

Mke wa Samidoh aliye nchini Marekani, Bi Edday Nderitu, alisema matukio hayo ni dharau kwa wanawe.

“Jambo nzuri ni kwamba watoto hao ambao amewadharau, atakuwa akiwaona kwenye mitandao ya kijamii kama watu asiowafahamu,” alisema Bi Nderitu ambaye kwa sasa yuko Marekani na watoto wake watatu.

Inaaminika kuwa nyumba hiyo ambayo imezua cheche miongoni mwa mashabiki, Samidoh aliijenga kabla ya kuwepo na uhusiano na Bi Nyamu ambaye wana watoto wawili naye.

  • Tags

You can share this post!

Madereva watundu wanaoibia wachuuzi

Ndindi Nyoro: Wakosoaji wa Ruto wamefanyia Kenya nini?

T L