• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 11:33 PM
Babu Owino asema hajutii kuvuta bangi, kutumia mihadarati awali

Babu Owino asema hajutii kuvuta bangi, kutumia mihadarati awali

NA FRIDAH OKACHI

MBUNGE wa Embakasi Mashariki Paul Ongili maarufu Babu Owino, hanywi tena pombe wala kutumia dawa za kulevya baada ya kuacha uraibu huo Januari 2020. 

Katika mahojiano kwenye video moja iliyopeperushwa mitandaoni, Bw Owino anaeleza safari yake ya kuacha kutumia dawa za kulevya na pombe.

“Sijutii kupitia njia hiyo, sababu imenifanya nielewe sio vizuri kujihusisha na matumizi ya dawa za kulevya,” alisema mbunge huyo.

“Nimekunywa pombe, nimetafuna miraa, nimetumia kokeni, nimevuta bangi, nimekunywa chang’aa, busaa, muratina hivi vyote nimetumia,” aliendelea kusema.

Bw Owino alisema vijana wengi hutumia muda wao mwingi kujifurahisha wanapotumia dawa za kulevya.

Hali hiyo imeweza kumfungua macho na kumwonyesha sio vyema kuishi kwenye uraibu huo ambao ungemsababishia kupoteza mwelekeo na kukosa kufanikisha ndoto ya kuwa kiongozi mtajika.

Uamuzi wake wa kuacha kutumia pombe na dawa za kulevya ni kutaka maisha yake kuimarika, anasema.

“Niliamua kufuata mkondo mmoja wa maisha. Wakati unaambia akili yako utanataka kufanya jambo fulani, utalifanya. Nilifanya uamuzi huo nikijua nitawacha. Sikuwahi kuenda katika kituo chochote,” alisema Bw Owino.

Alisema maisha hayo yalimgharimu na kufanya maamuzi mabovu.

Uamuzi huo ni pamoja na kuhusishwa kwenye tukio la kumpiga risasi DJ Evolve katika eneo la burudani mjini Nairobi.

Hali ambayo ilimpelekea Dj Evolve kukosa kuzungumza na kutembea kwa muda huku akitegemea jamaa wake wa karibu kumshughulikia.

Bw Owino amepanda ngazi kadhaa za uongozi hadi kuchaguliwa kuwa mbunge kwa mara ya pili eneo bunge la Embakasi Mashariki.

  • Tags

You can share this post!

Raila amwambia Ruto aache kutangatanga, achape kazi

Jinsi mikakati ya serikali kuhusu ushuru inavyokunywa maji...

T L