• Nairobi
  • Last Updated May 10th, 2024 5:15 PM
Raila amwambia Ruto aache kutangatanga, achape kazi

Raila amwambia Ruto aache kutangatanga, achape kazi

Na WINNIE ATIENO

KINARA wa ODM, Bw Raila Odinga amemsihi Rais William Ruto kukomesha ziara zake za kigeni na kuwafanyia kazi Wakenya.

Bw Odinga alisema Rais Ruto alitoa ahadi nyingi na Wakenya wanasubiri aanze kuzitimiza.

Wakati huo huo, kiongozi huyo wa Upinzani alisema Azimio haitafanya mkataba wowote na serikali endapo haitatatua changamoto zinazowakabili Wakenya hasa gharama ya maisha.

“Tunataka serikali kuu kutekeleza wajibu wake badala ya kusema maneno matupu na domo kaya. Gharama ya maisha bado imepanda.

Bei ya unga bado iko juu, petroli, sukari na umeme na bado Rais anaendelea kutoa ahadi,” alisema Bw Odinga.

Bw Odinga alisema ziara za Bw Ruto ughaibuni hazijasaidia Wakenya akimtaja kama Rais wa kutangatanga mataifa ya kigeni.

“Sisi kama Azimio tumesimama imara, na tumesema hatuwezi kufanya mkataba wowote ambao hautaweka mambo ya huduma ya wananchi mbele. Lazima gharama ya maisha ishuke,” alisema Bw Odinga.

Alisema uongozi wa Rais Ruto umeshindwa kutekeleza ahadi walizotoa wakati wa kampeni.

Kinara huyo wa ODM alimtaja Rais kuwa mtu wa mdomo mtamu ambaye anashindwa kuwajibika.

“Hawa ni watu wa maneno matamu na porojo nyingi. Mdomo mtamu sio chakula wananchi wanateseka wengine wanalala njaa. Ndio maana nimewaambia badala ya kuzururazurura hapa na pale watafuta namna ya kuwafanyia wakenya kazi ili kushukisha gharama ya maisha,” alisema.

Akiongea katika hospitali ya Port Reitz alipokuwa akielekea uwanja wa ndege wa Moi, Bw Odinga alisema shirika la utafiti la Infotrack lilifanya kura ya maoni kuhusu huduma nchini.

  • Tags

You can share this post!

Davis Chirchir: Huenda lita moja ya petroli ikagonga Sh300

Babu Owino asema hajutii kuvuta bangi, kutumia mihadarati...

T L