• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 11:33 PM
Brown Mauzo na Vera Sidika kukutana uso kwa macho baada ya kurushiana cheche mtandaoni

Brown Mauzo na Vera Sidika kukutana uso kwa macho baada ya kurushiana cheche mtandaoni

NA FRIDAH OKACHI

SOSHIOLAITI Vera Sidika na mwanamuziki Brown Mauzo wanatarajiwa kukutana kwenye hafla moja wikendi hii ijayo.

Hii itakuwa ni hafla ya kwanza wawili hao kukutana baada ya kurushiana cheche za maneno kwenye mitandao ya kijamii.

Mashabiki wamekuwa na mengi ya kuchangia kuhusu habari hizo. Tunaanza na Eph_inie.

“Eeeiiyy!!chiiiiiii! Umesema mambo ya watu wawili tusiyaingilie,” akaandika Eph_inie.

Naye Mariontasmani akaandika: “Siku nyingine tujikumbushe si vyema kushughulika na biashara za watu. Ona sasa kimeturamba.”

Boobtape- city: “Mbona mnafanya wadaku wakae waongo?”

Katika chapisho lake, Mauzo kwenye ukurasa wa Instagram alisema tamasha hilo litafanyika eneo la Jamii Executive Gardens mjini Mwea.

Mwanamuziki huyo na Vera wameratibiwa kuwa wageni maalum tangu kutengana kwao.

Kwenye bango hilo, pia mwanamuziki wa kufokafoka Khaligraph Jones, mburudishaji kwenye kilabu MC Gogo na kikundi cha muziki wa kufoka cha Wakadinali watanogesha hafla.

“Wafalme na malkia, usiku wa Jumamosi hii nitakuwa Jamii Executive Gardens. Njooni kwenye sherehe na Bw Loverman. Msiniangushe kwa hilo!” alichapisha Bw Mauzo.

Kukutana kwa wawili hao mjini Mwea kunakotarajiwa, kumewafanya mashabiki wa pande zote mbili kutaka kujua jinsi mambo yatakavyokuwa jukwaani na pia kutathmini kiwango cha burudani kutoka kwa wawili hao hata baada ya penzi kuingia mdudu na kila mmoja kuenda zake.

Wawili hao walitangaza kutengana mwishoni mwa Agosti 2023.

Juma lililopita, walionekana wakirushiana cheche za maneno kwenye mtandao wa Instagram.

Vera alidai aliandaa karamu akamwalika Bw Mauzo ambaye alikosa kufika.

Mnamo Novemba 5, 2023, Bw Mauzo alichapisha haya katika kurasa zake za mitandao ya kijamii, kuashiria kuwa huenda amepata mpenzi mwingine.

“Lengo langu ni kujenga na wewe, kukua na wewe na kukuoa. Mimi sikuchumbii kupoteza muda. Ninaona kila ninachotaka kwako mpenzi wangu,” alisema Bw Mauzo.

  • Tags

You can share this post!

DPP apewa siku 14 kuandaa ushahidi katika kesi ya...

Kizaazaa video zilizo na ushahidi wa kumtetea Mwangaza...

T L