• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 5:50 AM
Ex wa Bahati, Yvette Obura ‘aringisha’ kadudu Nissan Note akisema ni bidii yake

Ex wa Bahati, Yvette Obura ‘aringisha’ kadudu Nissan Note akisema ni bidii yake

NA FRIDAH OKACHI

MFANYABIASHARA Yvette Obura apiga hatua kwa kununua gari ambalo limesisimua mashabiki kwenye mtandao wa Instagram.

Mama huyo wa mtoto mmoja na ambaye pia alikuwa mpenzi wa kitambo wa Kelvin Kioko almaarufu Bahati, alionyesha picha ya gari akiwa amesimama mbele ya aina la Nissan Note yenye rangi ya samawati.

Novemba 8, 2023, alichapisha ujumbe ambao ulionekana kusimumua mashabiki wake.

“Pesa kidogo nishanunua kadudu,” aliandika Bi Yvette.

Mashabiki wake wakiwemo wanamziki kadhaa walimpongeza huku wengine wakimkejeli kwa hatua hiyo.

Shabiki mmoja wa Instagram alidai kuwa gari hilo alipata kutoka kwa mwanamuziki Bahati ambaye alikuwa amemnunulia mkewe, Diana Marua gari lingine aina ya Range Rover.

Rosemary irungu: Hiyo ndiyo zawadi Bahati aliongezewa baada ya kunua range.

Bi Yvette alionyesha wazi hatopendezwa na maoni hayo.

“Mama mzima kama wewe huna akili!” Alijibu Bi Yvette.

Shabiki mwingine aliweza kuwakejeli wafuasi wa Diana, akifurahia hatua aliyofanya Bi Yvette.

isirengo: Hongera! Bandilisha rangi kabla team Diana waanze ooh! sijui umecopy zawadi nambari ya  7 bla bla bla…

eunnycharles: Hii ni biashara tuu, mum Mueni ana gari kubwa zaidi ya hili.

Baadhi ya watu wenye umaarufu kwenye fani ya uimbaji vilevile waliweza kufurahia alichofanya Bi Yvette, hawa hapa wakipongeza hatua hiyo.

mrseedofficial: Ulicheza wimbo upi hapo ya kwanza…Nafurahia bidii yako, Hongera.

 officialkinuthia: Karibu kwa kundi la Note.

nipha.001: Wanawake wanatia bidii kutafuta vyao, Nawasherekea kwa kia hatua, Hongera.

Mama huyo siku za hivi karibuni alionekana kutoelewana na familia yake mwanamuziki Bahati mahali ambapo mwanawe alikuwa akiishi na kusomea. Bi Yvette aichukua hatua ya kumtoa na kumtenganisha na familia ya bahati mapema Februari, 2023.

Mfanyabiashara huyo na mkewe Bahati waionekana kurushiana cheche, huku Diana akimlaumu kwa kukosa kuwa na wema.

Yvette ambaye alikuwa akisherekea siku yake ya kuzaliwa Machi 11, 2023 aliambia mashabiki kuwa kunai le heshima anajipa, hii ni baada ya wawili hao kukosa kuonekana kwa muda pamoja na mwanawe Yvette kukosa kutangamana na ndugu zake watatu.

  • Tags

You can share this post!

Wito mwongozo maalum wa akili mwigo AI utumike kufanikisha...

Seneta Karen Nyamu asimulia jinsi penzi lake kwa Samidoh ni...

T L