• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 7:50 AM
Seneta Karen Nyamu asimulia jinsi penzi lake kwa Samidoh ni gluu ‘permanent’

Seneta Karen Nyamu asimulia jinsi penzi lake kwa Samidoh ni gluu ‘permanent’

NA FRIDAH OKACHI

SENETA maalum Karen Nyamu amefichua amewahi kujaribu kujitoa kwenye uhusiano wa kimapenzi na mwanamuziki Samuel Muchoki almaarufu Samidoh bila mafanikio.

Akizungumza kwenye mahojiano na Convo katika mtandao wa YouTube, seneta huyo alisema kabla mambo yao hayajajulikana hadharani, alijaribu kusitisha mahusiano hayo kutokana na shinikizo kwenye mitandao ya kijamii na kumhurumia mke wa mwimbaji huyo wa nyimbo za Mugithi, Edday Nderitu.

Waongazaji wa mahojiano hayo walikuwa ni Silver Spook na Patrick Igunza.

“Nimejaribu kuondoka kwa uhusiano huo Si kwamba sijawahi kujaribu kupigana nayo kwa sababu ya presha na nini na nini… na pia nikiwa mtu mzuri, kuna wakati ningeona hali jinsi ilivyokuwa haikuwa nzuri. Nilitafakari ni vipi kuhusu mtu mwingine lakini hamjui mambo ya roho. Nyinyi hamjui vizuri), ogopa roho! Humjui vizuri,” alisimulia Bi Nyamu.

Seneta huyo kwa pamoja na Samidoh wamejaliwa watoto wawili.

Anashikilia msukumo wa damu na mvuto kwa mwanamuziki huyo ulikataa.

“Huu uhusiano ulinata kama gluu tokea azali na tukawa na mwingiliano,” aliendelea kusimulia seneta huyo.

Alisema kuwa uhusiano wao ni muunganisho wa asili tu na akaweka wazi kwamba ni kitu kinachompa furaha. Pia alibainisha kuwa hayuko kwenye uhusiano kwa sababu ya pesa kwani wote wamejaliwa mali.

“Mambo ya roho! Nilijaribu kukwepa, lakini nikasema mazee acha basi sasa penzi likoleze kwa sababu nilijaribu kujitoa nikashindwa,” akaweka mambo wazi.

Kulingana na Bi Nyamu, alimpenda mwanamuziki huyo kutokana na kuwa ni mtu mkweli.

Mwanasiasa huyo alisema kuwa wakati wa kwenda kwenye vyumba vya burudani angemwonea kwa umbali bila kumfuata jinsi wengine walivyokuwa wakimfuata.

“Ni chali mpoa, ana roho poa, vibe poa na hajifanyi au kuwa na maringo. Pia ananiambia maneno matamu ambayo nimemwambia ni wazi sitawahi kuyasikia kutoka kwa mwingine maishani mwangu,” akasimulia.

Mwanasiasa huyo amesifia mpenzi wake akisema anaona raha kwelikweli kuwa kwenye uhusiano huo.

“Ana mapenzi tele, kuna wakati anakuja nyumbani akiwa na maua, pia anapiga simu ananikujia na tuende kubarizi tukiwa wawili tu na baada ya kula na kunywa basi tunarejea nyumbani,” akasema.

  • Tags

You can share this post!

Ex wa Bahati, Yvette Obura ‘aringisha’ kadudu...

Haya ndiyo mafanikio ya Kenya Kwanza, Rais Ruto aambia...

T L