• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 7:50 PM
Natalie: Niliachwa kwa sababu ya maradhi

Natalie: Niliachwa kwa sababu ya maradhi

NA RAJAB ZAWADI

KUACHWA na kuachana kupo, au sio bwana?

Ila kuna dizaini nyingine za kuachwa zimwachazo mtu na vidonda vya roho.

Mchekeshaji na mtangazaji Natalie Githinji amekuwa akiuguza vidonda hivyo vya rohoni baada ya kuachwa  na mpenzi wake eti kisa hawezi kumsitiri inavyotakiwa.

Toka 2016, Natalie amekuwa akiugua ugonjwa matata wa Endometriosis ambao humtatiza sana kwenye vipindi vyake vya hedhi.

Ugonjwa huu huwa ni vidonda kwenye chungu cha uzazi na huwa ni uchungu balaa.

Zimwamliapo, Natalie huzidiwa na maumivu makali kiasi kwamba hata kutembea, kuoga au kufanya anayofaa kufanya na mpenzi wake, yeye hushindwa.

Mara nyingi mamake ndiye amekuwa akimpa msaada wa kumtakatisha pale anaposhindwa kujiogesha.

“Ugonjwa huu umeathiri mambo mengi sana kwenye maisha yangu. Nimeshatorokwa na mpenzi maana huwezi kumpa haki yake ya kimapenzi kutokana na uchungu mwingi unaosababishwa na Endo’. Mtu anashindwa kukuelewa anakuambia wewe kila siku unaumwa tu!” Natalie kafichua.

Maradhi haya anasema yamemkausha sana mfuko kwani amezunguka takribani katika kila tabibu akisaka msaada lakini bado hajafanikiwa.

IMEKUSANYWA NA SINDA MATIKO

  • Tags

You can share this post!

Kenya yalipa Sh10 bilioni za riba ya Eurobond

Mwalimu anayedaiwa kuwaua wanawe atiwa mbaroni

T L