• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 11:33 PM
Nimerudi soko, atangaza Akothee akithibitisha kwa mara ya kwanza kuachana na mzungu

Nimerudi soko, atangaza Akothee akithibitisha kwa mara ya kwanza kuachana na mzungu

MERCY KOSKEI na FRIDAH OKACHI

Mwimbaji na mfanyabiashara Esther Akoth almaarufu Akothee amethibitisha kuwa ndoa yake na Denis Schweizer kwa jina la utani ‘Omosh’ ilitamatika miezi mitano iliyopita.

Akothee alithibitisha madai ambayo yamekuwa yakienea kwa muda mrefu Jumanne Octoba 31,2023 kupitia mtandao wa kijamii.

Kupitia kipindi cha moja kwa moja kwa mtandao wake wa TikTok, Akothee alifichua kuwa walitengana na Omosh mnamo mwezi wa Juni, akisema uhusiano huo haukumsaidia na hangeweza kulazimisha.

Akothee alifichua  kuwa aligundua baadhi ya mambo kuhusu mumewe wakati wa honeymoon yao ambayo hakuweza kuyastahimili, hivyo kuamua kuondoka.

“Ndoa yetu haipo tena. Ningependa kuwaambia kwamba nilijiondoa kwenye uhusiano huo mnamo Juni. Sitaeleza kwa undani, nilifurahia ndoa yangu; Nilifurahia harusi yangu. Sijutii chochote. Nilifanya harusi yangu siku ya kuzaliwa kwangu, sina majuto yoyote,” alisema.

Mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 43 alifichua kwamba aligundua mambo kadhaa ambayo hakujua hapo awali.

Hata hivyo, alisema kwamba hakumwambia Omosh kuhusu uamuzi wake wakati huo, akisema kuwa alimdanganya kuwa hatamwacha.

“Mimi ni mtu ambaye silazimishi mambo. Wakati mambo hayaendi vizuri kwangu, najitoa tu. Kawaida huwa natoka kwenye mahusiano nikiwa bado kwenye mahusiano, nikiwa kwenye honeymoon niligundua baadhi ya mambo ambayo sikuweza kuendelea nayo, Julai akaniuliza kama nitamuacha lakini nikamwambia hapana, baby, nakupenda lakini nilikuwa tayari nimeondoka,” alidokeza.

Hata hivyo msanii huyo aliweza kuzungumzia uzuri wa Omosh, akisema alikuja maishani mwake wakati alikuwa anapitia mapito mengi. Anasema Omosh alimpa kile alihitaji na wakati kulikuwepo na vita kwa familia yake, Omosh alikuwa pale.

Mfanyabiashara huyo, siku za hivi karibuni alitishia kuwachukulia wanabloga hatua ya kisheria iwapo wangemhusisha Denis Schweizer kwenye taarifa zozote.

Pia kulikuwepo na tetesi kuwa jamaa huyo anatoka taifa la Pakistan, madai ambayo alipinga vikali kwa kuchapisha picha ya cheti chake, kilichoonyesha kuwa ni raia wa Uswizi.

Mwimbaji huyo aliweka wazi kuwa sasa yuko singo, akibainisha kuwa hakuna wakati ataruhusu mwanaume kumuathiri kisaikolojia.

  • Tags

You can share this post!

Gachagua arejea nchini kimya kimya na kuongoza mkutano...

Wazazi waonywa dhidi ya kuruhusu watoto wao kufanya...

T L