• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 12:38 PM
Rapudo athibitisha kutengana na Amber Ray akilaumu ‘uchizi’ kutokana na ulevi

Rapudo athibitisha kutengana na Amber Ray akilaumu ‘uchizi’ kutokana na ulevi

NA MERCY KOSKEI

KENNEDY Rapudo, mpenziwe Faith Makau almaarufu Amber Ray, hatimaye amezungumza wiki moja baada ya madai kuibuka mtandaoni kwamba wawili hao wametengana.

Rapudo alikiri kuwa mambo hayako sawa kati yake na mpenziwe Amber Ray.

Mnamo Oktoba 16, 2023, kupitia mtandao wake wa kijamii ya Intragram, mfanyabiashara huyo alikiri kumshambulia mpenziwe, huku akionyesha majuto kwa kitendo hicho na kuthibitisha kutengana kwao.

“Kama ndoa yoyote, tumekuwa na nyakati za misukosuko kumaanisha yetu pia si kamilifu. Mengi yamesemwa lakini sikuwa na nguvu ya kuyashughulikia,” aliandika.

Akaongeza: “Ndiyo, tumetengana kutokana na tukio lililotokea tukiwa walevi usiku wa Oktoba 13. Ni tukio ambalo halipaswi kutokea na ninajuta sana kwamba lilimtokea mtu ambaye niliapa kumlinda na kumpenda kwa yote niliyokuwa nayo.”

Kisha akarejelea machapisho ya kihisia ya Amber kuhusu suala hilo, ambapo alizungumza kuhusu unyanyasaji wa kinyumbani, akisisitiza kwamba hili lilikuwa tukio la kwanza.

“Tukio moja la pekee halimaanishi kuwa mimi ni mtu mwenye jeuri; sijawahi kuwa na sitakuwa! Ninalea wasichana wawili warembo na sitawahi kutetea unyanyasaji wowote wa kinyumbani au unyanyasaji wa kijinsia,” aliandika.

Rapudo alisema kuwa ataendelea kuwalea watoto wake kwa njia bora jinsi awezavyo na kupigania familia yake nje ya mitandao ya kijamii akiongeza kuwa anajutia kitendo hicho.

Inasemekana kuwa Amber Ray alitoka nyumbani na kuvua pete ya uchumba baada ya kutengana.

Alipokuwa akihudhuria tamasha kwenye kilabu kimoja wikendi, aliibua ucheshi kuhusu suala hilo, akiwaomba mashabiki kuhudhuria sherehe na “mtu ambaye amevunjwa moyo.”

Alipozungumza kuhusu kutengana kwake na Rapudo wiki iliyopita, aliwaambia wafuasi wake milioni 1.9 wa Instagram kwamba “inaumiza imani yako kuharibiwa kwa njia ambazo huwezi kujieleza kwa maneno.”

  • Tags

You can share this post!

Spika Kingi asalimu amri ya mahakama na kumruhusu Seneta...

Juhudi kuhifadhi na kukuza vyakula vya kiasili 

T L