• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 10:50 AM
Barobaro ajitokeza akidai yeye ni mtoto wa KRG the Don

Barobaro ajitokeza akidai yeye ni mtoto wa KRG the Don

NA MERCY KOSKEI

MVULANA mwenye umri wa miaka 18 amejitokeza na kudai kuwa msanii KRG the Don ni babake.

Hii inajiri baada ya mwanamuziki huyo kujipata kwa kisa kingine, ambapo inasemekana kuwa ametelekeza majukumu ya mwanawe msichana wa miaka 19.

Akizungumza wakati wa mahojiano na Vincent Mboya, kupitia taarifa zake za You Tube, kijana huyo aliyetambulika kama Brighder, alidai kuwa msanii huyo ni babake na alikuwa tayari kuthibitisha madai yake.

Brighder ambaye ni mwanafunzi katika taasisi moja jijini Nairobi, alidai kuwa hajawahi kutana na babake na kuwa ana matumaini kupatana naye ana kwa ana.

“Mama hushinda akisema kuwa babangu ni msaani mkubwa nchini  Kenya kisha ananyamaza, lakini wiki iliyopita kulikuwa na shida kwa sababu babangu alikuwa anamulikwa mitandaoni kwa madai ya kutelekeza majukumu,” alimwelezea Mboya.

“Kama atataka vipimo vya msimbo jeni (DNA) ama nitoe stakabadhi zangu zitakazoonyesha kuwa ni babangu, niko tayari kufanya hivyo. Baba – wakati utataka ushahidi kamili utanieleza,” aliongeza.

Akionekana kuwa na wakati mgumu kueleza ni kwa nini alichagua kufichua wakati huu, alidai kwamba alikuwa akiheshimu matakwa ya babake alipomtaka yeyote anayehisi kuwa wana uhusiano wa karibu ajitokeze.

Huku akikana kuwa ilikuwa mbinu kutafuta ufuasi mkubwa mitandaoni, Brigher alibainisha kuwa alikuwa akitafuta tu mapenzi ya baba na kutambuliwa na babake.

Alijitetea akisema; “Ninachotaka ni kupata mapenzi ya baba mzazi, anitambue. Sifuati pesa zake.”

Kwa sasa, amemtaka msanii huyo kumtafuta ili wawe na kikao kuzungumza waki pekee yao, huku akisisitiza kuwa yuko tayari kwa vipimo vya DNA .

Hapo awali, msanii huyo alibanwa na mwanamke mwingine kwa jina Susan Kinyanjui aliyedai kuwa walikuwa na mtoto naye.

Susan alimshutumu mwanamuziki huyo kwa kukosa kutimiza wajibu wake kama baba kwa binti yao Yvonne.

  • Tags

You can share this post!

Serikali yamtuza Faith Kipyegon Sh5 milioni na nyumba ya...

Kabale Tache ateuliwa Afisa Mkuu Mtendaji wa NLC

T L