NA MARGARET MAINA
ZUCCHINI huwa na virutubisho vingi. Ingawa zucchini mara nyingi huchukuliwa kuwa mboga, huainishwa kibotania kama tunda. Zifuatazo ni baadhi ya sifa za zucchini.
Muda wa kuandaa: Dakika 10
Muda wa mapishi: Dakika 40
Walaji: 4
Vinavyohitajika
kikombe 1 zucchini.
kikombe 1 cha karoti (menya na saga)
siagi kikombe ½ (iliyoyeyuka)
kikombe ¼ cha sukari nyeupe
kikombe ½ cha sukari ya kahawia
mayai 2
dondoo la vanilla kijiko 1
kikombe 1 ½ unga wa ngano
mdalasini kijiko 1
baking soda kiasi cha kijiko 1 cha kukorogea chai
kijiko ½ cha chumvi
kikombe cha karanga (kilichokatwa)
kikombe nusu chipsi tamu za chokoleti (hiari)
Maelekezo
Osha na suuza Zucchini na karoti.
Koroga kwa pamoja zucchini, karoti, siagi iliyopozwa (iliyoyeyuka), sukari, mayai, na vanilla.
Katika bakuli jingine, changanya unga wa ngano, mdalasini, soda ya kuoka na chumvi.
Changanya viungo kavu na mchanganyiko wa zucchini. Koroga hadi vichanganyike tu.
Kisha koroga karanga na chokoleti, ikiwa unatumia.
Mimina unga kwenye sufuria ya kuokea mkate iliyopakwa siagi.
Oka kwa digrii 180 kwa muda wa dakika 40 hadi uma ukiingizwa katikati utoke ukiwa safi.
Subiri mkate upoe kabla ya kula.