Na MARGARET MAINA
SUNGURA ni mnyama ambaye faida ziambatanazo na ufugaji wake ni nyingi.
Nyama ya sungura ina protini nyingi na mafuta kidogo ikilinganishwa na nyama ya kondoo na kadhalika. Kwa hiyo, nyama ya sungura ni nzuri kuliwa na watu ambao wana magonjwa mbalimbali.
Ina protini nyingi
Nyama ya sungura huongoza kwa kuwa na kiwango kikubwa cha protini ambayo ni asilimia 21 ikifatiwa na ile ya kuku yenye asilimia 18.
Mpaka sasa hakuna nyama yenye kiwango kuzidi hiki. Ulaji wa nyama ya sungura unakupa protini nyingi zaidi kuliko nyama nyingine yoyote ambayo unaweza kuipata.
Ina kiwango kidogo cha lehemu
Kwa kutumia nyama ya sungura unakuwa unaepuka madhara hayo kwa kiwango kikubwa.
Ina kiwango kidogo cha sodiamu hivyo ni nyama bora kwa ajili ya watu wenye matatizo ya ugonjwa wa moyo
Nyama ya sungura ni nyeupe. Nyama nyekundu huwa na Nucleic aside nyingi ambazo huchangia Uric acid nyingi ambayo katika mwili wa mlaji inatakiwa ikae katika hali ya kumiminika na mwili ukishindwa au kuzidiwa hizi asidi hutengeneza chembe chembe za maungio (joints) na kusababisha maumivu (gout). Pia nyama nyekundu huwa na lipoprotein ambayo huchochea utengenezaji wa lehemu yenye madhara. Kwa kula nyama ya sungura, haya yote yanaepukika.
Haina mafuta mengi
Na ina mafuta ambayo hayana madhara mwilini mwa mtumiaji.
TANBIHI
Baadhi ya watu hawali nyama ya sungura kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na mafundisho ya kidini.