• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 8:55 PM
Jifunze kuandaa pankeki tamu za matunda ya blueberries

Jifunze kuandaa pankeki tamu za matunda ya blueberries

Na WINNIE ONYANDO

WAFURAHISHE uwapendao kwa kuwaandalia pankeki za matunda ya blueberry.

Kando na kuwa rahisi kuandaliwa, aina hii ya keki huwa na utamu usiopimika

Vinavyohitajika

Kikombe 1 cha unga wa ngano

Vijiko 2 vya sukari

Vijiko 2 vya hamira

Chumvi kijiko nusu (kiasi unayopenda)

Kikombe 1 cha maziwa

Vijiko 2 vya siagi isyo na chumvi, iliyoyeyuka, au mafuta

Yai 1

Kijiko 1 cha mafuta

Pakiti 1 ya matunda ya blueberry

Maandalizi

Katika bakuli ndogo, changanya unga, sukari, hamira na chumvi.

Kisha changanya maziwa, siagi / mafuta na yai kwenye bakuli tofauti.

Weka mchanganyiko hizo mbili kwenye bakuli moja kasha uongeze maziwa kwenye mchanganyiko (usichanganye), wacha kwa muda wa dakika tano ili yayeyuke pole pole.

Weka sufuria safi ya kupikia kwenye moto ya kati na utie mafuta.

Tia mchanganyiko wako kwa utaratibu kwenye sufuria na uhakikishe kuwa kila pankeki zako zina umbo mviringo.

Kabla ya kuweka kila pankeki kwenye sufuria ya kupikia, tia vijiko viwili ya siagi.

Ongeza matunda ya Blueberries chache kwenye kwenye kila pankeki.

Pika kwa dakila moja au mbili.

Pindua kwa uangalifu kwa kukitumia kijiko chembamba, na upike hadi uwe hudhurungi kila upande.

Weka kwenye karatasi ya kuoka au sinia kisha ufunike na karatasi ya aluminium. Weka kwenye oveni kwa dakika mbili.

You can share this post!

Makala ya msanii wa nyimbo za injili Mary Njuguna

Shaqiri atia saini mkataba wa miaka mitatu kambini mwa Lyon