Na MARGARET MAINA
Muda wa kuandaa: Dakika 15
Muda wa mapishi: Dakika 30
Walaji: 4
Vinavyohitajika
Maelekezo
Osha kuku vizuri kisha kata mnofu uwe vipande kwa maumbo uyapendayo.
Weka kwa kuku viungo vyako kama tangawizi, kitunguu saumu, ndimu moja, na chicken masala vijiko viwili kisha changanya vizuri kabla ya kuweka kwenye jokofu kwa saa si chini ya mbili.
Kata karoti, pilipili mboga na kitunguu maji kwa urefu au umbo upendalo ila viwe vipande vikubwa vinavyoonekana baada ya kuiva.
Saga nyanya na iweke kwenye bakuli.
Chukua kikaangio, mimina mafuta hapo na yaache yapate moto wa wastani.
Anza kukaanga vipande vya kuku taratibu mpaka viive.
Tumia karai. Kwanza punguza mafuta ubakisha mafuta kiasi kwa ajili ya kukaanga viungo vilivyobakia.
Anza kukaanga kitunguu kisha weka pilipili mboga na malizia na karoti ila usikaange kwa muda mrefu kwa sababu havitakiwi kuiva sana.
Weka nyanya ulizosaga, koroga na malizia kwa kuweka chumvi, masala, nyanya ya kopo, pilipili na ile ndimu kipande kilichobakia.
Ingiza kwenye kikaangio vipande vya kuku na ukoroge kidogo ili navyo viungo vienee kisha epua na upakue kwenye sahani.
Chakula hiki kile pamoja na viazi, ndizi za kukaanga, ndizi za kuchoma, wali au chapati.
Angalizo
Hakikisha unapikia kwenye karai.
Usiweke maji wala nyanya nyingi wakati ukipika.
Rosti halitakiwi kuwa jingi; yatakuwa sio makange ni mchuzi sasa.
Kama huna kuku unaweza kupika kwa nyama ya ngo’mbe, mbuzi, samaki wa kukaanga na kadhalika.