• Nairobi
  • Last Updated May 6th, 2024 10:55 AM
Kajala awakataa wanaume wa Kenya kwa kumchezea ‘kalongolongo’   

Kajala awakataa wanaume wa Kenya kwa kumchezea ‘kalongolongo’  

NA JOHN KIMWERE

KATI ya waigizaji mahiri wa filamu za bongo, Fridah Kajala Masanja amesema kamwe hatoingia kwenye mahusiano ya kimapenzi na wanaume wa Kenya.

Kupitia mtandao wake wa Instagram, Kajala mwenye umri wa miaka 40, ambaye ni mpenzi wa zamani wa msanii Harmonize amewaonya wanaume wa Kenya akiwataka wakome kuingia kwenye safu yake ya jumbe kwa nia ya kutongozana.

“Nipo singo lakini sipo tayari kuingia kwenye mahusiano na mwanaume yeyote kutoka Kenya, nimewachoka,” akasema msanii huyo.

Aliongeza kuwa amevunjwa moyo na wanaume wa Kenya, na kwamba hataki kuumizwa na kuuguza majeraha ya moyo tena.

Kajala amefunguka hayo miezi kadhaa baada ya ziara yake hapa nchini, ambapo alitumia jukwaa la matembezi yake kutangaza kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na mwanaume wa Kenya.

Wakenya wengi walikuwa wanasubiria Kajala kumtangaza rasmi jamaa aliyekuwa anachumbiana naye.

Kajala ambaye kando na uigizaji, ni mwanamitindo na mwanabishara nchini Tanzania aliachana na Harmonize aliyemchamba kuwa na mchepuko.

Chapisho hilo la Kajala, mama wa mtoto mmoja, Paula limesababisha mjadala mkubwa kwenye mitandao ya kijamii.

Baadhi wanamuunga mkono, huku wengine wakimlaani kwa kuwaponda wanaume wa Kenya.

  • Tags

You can share this post!

Urais: Cherargei alimwa na viongozi wa upinzani

Wabunge wa Azimio Magharibi wawashutumu Kuria na Ndii

T L